Tuesday, December 14, 2010

UCHAKACHUAJI WAGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI, KANSA NYINGINE INAYOITAFUNA CCM

UCHAKACHUAJI WAGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI, KANSA NYINGINE INAYOITAFUNA CCM.

Na Godfrey Mushi

WAKATI wa viongozi kuwazungusha na kuwahadaa wananchi kutokana na maamuzi yao katika michakato mbalimbali mara zinapotokea nafasi za kuwania nyadhifa kadhaa za uongozi,

iwe kupitia vyama vya siasa au sehemu ya serikali ni vyema ufikie kikomo kwa mantiki ya kuponya kirusi cha kansa kinachokitafuna Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa sasa.

Kauli zao,vitendo vyao na misimamo yao ni kama vimenaswa na kuhifadhiwa katika njia mbalimbali za mawasiliano.

Wananchi wa sasa wameamka,wanajua kinachoendelea dhidi ya uchakachuaji, wameonyesha  uthubutu kwa kuwagomea kwa kufanya maamuzi magumu, hakika wanaoendekeza ubazazi huo, kamwe hawawezi kuzuia. ni vyema waseme kweli wakati wote.

Tangu ulipoanza mchakato wa uchaguzi mkuu wa mwaka huu uliomalizika mwishoni mwa mweziOktoba,wagombea mbalimbali wamekuwa wakilalamika na kupaza sauti baada ya kuchakachuliwa kwa madai ya kigezo cha ukabila,udini na makundi.

Waliothubutu kujitokeza kuwania nafasi za ubunge na hata udiwani ambao walifanya hivyo kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania ibara ya 8 kifungu cha kwanza cha sheria ya mwaka 1984 ambayo inasema kuwa Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii,hawajaridhishwa na maamuzi yaliyofikiwa.

Sasa hivi gumzo katika vyombo vya habari na huko mitaani ni kuhusiana na mchezo mchafu wa uchakachuaji wa majina ya waliojitokeza kuwania kuteuliwa kugombea nafazi za U-meya,Wenyeviti wa Halmashauri na manaibu wao.

Baada ya wengi wao kubaini kwamba majina yao yalianza kuchakachuliwa kwa kuwekewa alama ndogo (dhaifu) katika ngazi za Wilaya hata kabla ya kupelekwa mkoani ambako njama za kuhakikisha hawafiki kokote zilitekelezwa kwa lengo la kuwakata makali,sasa zimegeuka kidonda kilichoanza kuota uvundo.

Njama hizo za kuwafifisha wanaooneka kuwa na nguvu kisiasa, zilitengenezwa hata kabla ya majina ya wagombea kufikishwa katika kikao cha Kamati ya Halmashuri Kuu ya CCM iliyokutana Desemba 10 mwaka huu Jijini Dar es Salaam.

Kamati hiyo (CC) ilikutana kwa ajili ya kujadili na kutoa maamuzi ya mwisho baada ya kupokea mapendekezo yaliyofikiwa katika ngazi za wilaya na mikoa.

Lakini katika hili la uchakachuaji nani alaumiwe kati ya kamati kuu na ngazi za Wilaya na Mikoa ambazo zilidanganya kwa kuchakachua taarifa au majina ya wagombea ambayo hayakufika kamati kuu na hata hayo yaliyopelekwa na kurejeshwa tayari kwa ajili ya kupigiwa kura yapo ambayo  yamegubikwa na dosari nyingi kutokana na udanganyifu uliofanywa katika ngazi za Wilaya na Mkoa.

Nimekuwa nikijiuliza mara nyingi ili kumaliza mkanganyiko na malalamiko haya ama pengine kuepusha migogoro ndani ya CCM ni kwa nini wajumbe wa Kamati kuu wanapopitia majina na mapendekezo toka mikoani, wasiangalie ama kuhoji iwapi mihutasari ya vikao vya ngazi hizo?

Kama viongozi waandamizi wa CCM wakibaini mapungufu hayo na kuwa wakali katika ukaguzi wa taarifa hasa mihutasari ya vikao vya kamati za siasa mikoani na Wilayani, ugonjwa huu wa saratani inayoitafuna CCM mithili ya siafu unaweza kutibu majeraha walao ya uchaguzi wa mameya,wenyeviti wa Halmashauri na manaibu wao.

Hakika,hiki ndicho kilichowasukuma baadhi ya wagombea wa nafasi za Umeya,Wenyeviti wa Halmashauri na manaibu wao ambao  wamechakachuliwa,kuamua kujiandaa kukabiliana na fedheha ya kushindwa kwao kutokana na kigezo cha ukabila ama udini.

Tayari maamuzi magumu yaliyotokana na mchujo huo, yameleta kizaa zaa na Madiwani wengine ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wametangaza kujiuzulu nyadhifa zao kutokana na mpasuko uliopo.

Mifano anuai ya waliochukua maamuzi magumu ni pamoja na madiwani wawili wa Wilaya ya Rorya mkoani Mara (CCM), Ongujo Wakibara kutoka Kata ya Mkoma na Lukio Ambogo ambaye ni diwani wa Kata ya Nyahongo.

Hawa wamelazimika kutangaza dhamira yao ya kuamua kuachia ngazi baada ya madiwani wenzao Charles Ochele,Yamo Odemba na Ongujo Wakibara, majina yao kukatwa na Kamati ya Siasa ya mkoa wa Mara.

Sakata hilo limetokea wiki chache tu baada ya Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Pius Msekwa kufika Rorya na kusikiliza malalamiko ya madiwani wapatao 10 waliokuwa wametishia kujiuzulu uanachama baada ya majina ya wagombea wenzao ambao wanatakiwa na wananchi kwa sasa kupigwa chini.

Wamefikia hatua hiyo kutokana na mpasuko wa kisiasa uliopo Wilayani humo lakini kubwa zaidi ni  kutoridhishwa na mchakato mzima wa kuchuja majina kwa maana ya kuwapa alama,kutoa mapendekezo na kuainisha vigezo kadhaa ikiwemo uadilifu, na namna ambavyo wamekitumikia chama chao.

Waliochukizwa na maamuzi hayo na kutangaza kujiuzulu wakipinga majina yao kuondolewa au kukatwa kwa misingi ya kuwalinda waliokuwepo katika madaraka hayo ya Umeya,Uenyekiti au Unaibu katika nafasi hizo nyeti ndani ya Halmashauri,ndio watakaorutubisha kirusi hicho cha Saratani kinachoitafuna CCM kama dhana ya ukweli ndani ya chama hicho itafunikwa.

Yapo madai ya baadhi ya viongozi wa CCM Wilaya ya Mbeya mjini kudaiwa kuongeza mpasuko wa kisiasa katika vita ya kumpata mgombea Umeya baada ya kudaiwa kuitisha mkutano wa kuwatisha madiwani wanaoonekana kuwa na dhamira ya kukisaliti chama kwa minajili ya kushawishi upigaji kura za maruhani.

Vivyo hivyo,mgongano wenye taswira ya namna hiyo umeripotiwa ndani ya CCM Wilaya ya Morogoro Mjini ambapo baadhi ya wagombea wamelalamikia kuhujumiwa katika vita hiyo na baadhi ya viongozi wa chama ngazi ya Wilaya.

Mambo kama hayo yametokea pia huko Iringa mjini ambako majina ya madiwani waliokuwa na nguvu kisiasa na waliokuwa wakitajwa tajwa mara kadhaa kwamba wanaweza kuwa sehemu ya mabadiliko, Mussa Wanguvu na Vitus Mushi majina yao yalikatwa.

Huko Tanga nako mambo hayakuwa shwari kwani Telesphori Chambo aliyekuwa akiwania nafasi ya Umeya alienguliwa kwa itikadi zinazohusishwa na udini.

Pengine naweza kusema ‘Uchakachuaji huu wa aina yake ni kirusi cha saratani kinachoitafuna CCM taratibu na walio madarakani wasipofikiri kwa haraka kukichoma kidudu hicho, watakaribisha kura za maruhani ambazo zitaiangamiza kwa kuigharumu zaidi muda mfupi ujao’.

Cha kushangaza,badala ya kutafuta mwarobaini wa kutibu kirusi hicho cha saratani kinachoitafuna CCM hivi sasa, Katibu mkuu wa CCM Taifa Yusuph Makamba amekaririwa akisema kuwa, uamuzi wa kugombea ulikuwa hiari yao na kujiuzulu pia ilikuwa ni hiari yao na kwamba CCM haita tetereka kwa uamuzi huo.

Kauli ya Makamba inakwenda sambamba na katiba ya chama hicho ambayo inasema wazi kwamba mtu atakoma kuwa kiongozi kwa kujiuzulu kwa hiari yake mwenyewe ama kwa kufukuzwa”.

Waswahili wanasema, ‘msafara wa nyoka hauna eskoti’…hivyo ni dhahiri kuwa wanaoendekeza dhamira katili ya kuwachakachua wenzao wasipate madaraka,hatuwaungi mkono wala kushabikia misimamo yao.

Ifike mahali,tutafakari kadhia hii ya uchakachuaji hadi lini? na ni nani angependa afanyiwe hivyo?

Godfrey Mushi ni Mwandishi wa Gazeti la Nipashe mkoani Iringa,anapatikana kwa simu namba 0767 535490 au barua pepe, ghandsome79@hotmail.com

MWISHO.



Friday, December 10, 2010

Vita ya Umeya yafunika nchi

Vita ya Umeya yafunika nchi

8th December 2010

Majeraha ya kura za maoni yaliyokigharimu Chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu uliopita huenda yakakiumiza zaidi katika hatua ya kusaka mameya, naibu meya na wenyeviti wa halmashauri nchini, kutokana na makundi kuibuka tena kwenye harakati za kuwania nafasi hizo.

Kuna kampeni za kidini na kikabila zinazofanyika chini kwa chini kwa wagombea kuchafuana kwa nia ya kujiweka kwenye nafasi nzuri ya uteuzi.

Katika Manispaa ya Iringa Mjini, kama uongozi hautafunika kombe ‘mwanaharamu’ apite, vita ya makundi na ukabila katika kumpata kiongozi huyo itazidi kukimega chama hicho.
Hadi sasa vigogo watano wamejitokeza kuwania nafasi hiyo akiwemo meya aliyemaliza muda wake, Amani Mwamwindi (Mlandege), Vitus Mushi (Mtwivila), Alphonce Mlagala (Ruaha), Mussa Wanguvu (Kihesa) na Daudi Albert (Mshindo).
Vigogo hao ndio wanasaka ridhaa ya chama chao kuwa meya wa Iringa Mjini.

Kinyang’anyiro kikali kipo kati ya Meya anayemaliza muda wake Amani Mwamwindi, Vitus Mushi aliyewahi kushika nafasi hiyo. Mushi pia alipata kuwa Mwenyekiti wa UVCCM mkoa huo miaka ya nyuma.
Kwa upande wa Manaibu Meya wamo Abubakar Mtamike (Gangilonga), Ally Mbata (Kitwiru) na Gervas Ndaki (Ilala).

Baadhi ya wananchi na wadau mbalimbali wametoa hadhari kwa CCM juu ya uteuzi wa atakayegombea nafasi ya umeya kuwa kama umakini hautatawala yale ya kwenye mpasuko wa kura za maoni kwenye kuwania ubunge wa Iringa Mjini yanaweza kujirudia.

Wana CCM na wadau mbalimbali mjini Iringa, wanasema wanataka meya atakayekuwa na uwezo wa kusimamia miradi ya maendeleo kwa kasi kubwa, kuandaa mipango ya kuiwezesha Manispaa ya Iringa kuwa Jiji, kuboresha miundombinu na kumaliza migogoro ya ardhi.
“Chama kinatakiwa kiwe makini sana katika kupitia uteuzi wa majina ya madiwani waliojitokeza kuwania kiti cha u-meya, kwa kuwa tunataka meya atakayetuandaa kuwa Jiji baadaye na mwenye maono ya mbali kimaendeleo, lakini pia mwenye nia thabiti ya kuibadili Iringa kimantiki, fursa za kiuchumi na hata ukuaji wake…hapa wakikosea tena ndio itakuwa maumivu makubwa,” anasema mmoja wa makada wa CCM mjini hapa.
Kumekuwepo na hisia za ukabila na udini mjini na sasa baadhi ya waliojitokeza wamefikia hatua ya kuchafuana kwa kutengenezeana majungu ili kumdhoofisha mpinzani wake asiteuliwe kugombea nafasi hiyo.
Hali ni hiyo karibu mikoa yote ambako watu waliojitokeza kuwania nafasi hiyo ni wenye majina makubwa na uwezo kifedha, maarufu na wale wa kawaida ambao hawavumi sana kwenye nyanja ya siasa.

Tayari Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, ametahadharisha kwamba wanachama wao wenye tuhuma hawatakuwa na nafasi katika kinyang’anyiro hicho.

Hata hivyo, wapo madiwani waliowahi kuwa mameya, manaibu meya na wenyeviti wa halmashauri ambao walituhumiwa kwa kujihusisha na ulaji rushwa wamechukua fomu kuomba tena kuchaguliwa kwa mara nyingine.
Baadhi yao waliwahi kutuhumiwa katika kashfa za uuzaji maeneo ya wazi, kuingia mikataba feki ya tenda za manispaa na halmashauri, pia wamechukua fomu za kuomba kugombea nafasi walizowahi kuwa nazo.
Katika Manispaa ya Musoma Mjini, Chadema kilikuwa kimejihakikishia ushindi mapema baada ya kutwaa kata nane kati ya 13 za Manispaa hiyo, na tayari kimetwaa nafasi ya meya na naibu meya baada ya diwani wa Nyamatare, Alex Malima Kifurura kupita bila kupingwa katika nafasi ya umeya wakati naibu wake, Angela Dereki wa Kata ya Kamnyonge naye amepita.

Mbunge wa jimbo hilo, Vincent Nyerere, alisema kwamba wanachosubiri wateule hao ni kuapishwa Desemba 17 mwaka huu kama madiwani ili waanze kutekeleza sera za chama chao.
Jijini Dar es Salaam, katika Manispaa ya Kinondoni, madiwani 20 wamejitokeza kuwania nafasi hiyo kwa tiketi ya CCM.

Miongoni mwa wagombea hao yupo Mkurugenzi wa Michezo ya Kubahatisha, Abbas Tarimba na Julian Martin Bujugo ambaye katika Baraza lililopita alipigania sana maeneo ya wazi kwa kutaka yasiuzwe na mwingine ni Katibu wa Siasa, Itikadi na Uenezi wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Songoro Mnyonge na Ibrahim Kisoky.
Wengine ni Issa Mtemvu, Charles Mgonja, Othman Kipeta, Christine Kirigiti, Majimasafi Shariff, John Mome Moro, Clement Boko, Yusuph Mwenda, Richard Chengula na Boniface Mnyachibwe.
Nafasi ya naibu meya inawaniwa na watu saba kati ya hao 20, akiwemo Rogate Mbowe, Husna Hemed na Charles Mgonja.
Katika Manispaa ya Ilala, pia mpambano ni mkali kwani wamejitosa aliyekuwa Naibu Meya katika baraza lililopita, Jerry Silaa (Ukonga), aliyekuwa mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Dk. Didas Massaburi (Kivukoni) na Hashimu Saggaf (Kariakoo).

Wagombea hawa ni kama wote wananguvu kisiasa kutokana na uzoefu na nafasi ambazo waliwahi kuzishika.
Temeke nako kuna mtindo wa kuchafuana ambapo baadhi ya wagombea wametuhumiana kugawa rushwa kwa viongozi wa CCM Wilaya na mkoa.

Suala hilo limeibua mpasuko, lakini tayari kuna taarifa kwamba waliotoa taarifa hizo kwa kuandika barua kwa Makamba pamoja na watuhimiwa, watahojiwa na Kamati Kuu ya CCM.
Wanaowania nafasi ya umeya wa Temeke ni tisa; ambao ni Anderson Charles (Kijichi), Hamis Msombo (Temeke), Noel Kipangule (Chang’ombe), Zena Mgaya (Tandika), Kenni Makinda (Vituka); huyu ni kaka wa Spika wa Bunge, Anne Makinda.
Wengine ni Hamis Kinyaka (Mtoni), Warda Hoja (Pemba Mnazi) na Francis Mtawa (Keko).
Mkoani Mbeya, CCM kamati ya siasa imependekeza majina matatu likiwemo la meya anayetetea nafasi hiyo, ambaye pia ni diwani wa Majengo, Athanas Kapunga, Dorr Issa Mohamed (Isanga) na Juma Simbeyange wa Kata ya Nsonho.
Chadema kimemsimamisha diwani wa Kata ya Forest, Boyd Mwabulanga, kuwania nafasi ya umeya wakati Diwani wa kata ya Ruanda Albert Hubert atawania nafasi ya Naibu Meya.

Mkoani Lindi waliojitokeza kwa tiketi ya CCM ni Frank Raphael Magali (Msinjahili), Suleiman Namkoma (Matopeni), Mohamed Lihumbo (Rahaleo) na Saidi Juma (Mbanja).­­­

Wanaowania unaibu meya ni Jamaldin Mandoa (Mingoyo) na Ismail Omary Mandambwe (Tandangongoro).
Kwa upande wa CUF aliyejitokeza ni Abdallah Mohd Khatau.

Katika Wilaya ya Nachingwea, wagombea wamejitokeza kuwania nafasi ya uenyekiti wa Halmashauri kwa tiketi ya CCM ni Chikawe Abdallah Mussa, Mpoyo Faida Kaisi, Mbinga Abdallah Mussa, Ngatupa Hamis Mohamed, Penengu Rabia, Juma Raphael na Saanane Petro. Umakamu wa mwenyekiti ni Salima Chiwalo Hassan.
Liwale wagombea watatu wamejitokeza kuwania nafasi ya uenyekiti wa Halmashauri ambao ni Abbas Matulilo, Hassan Myao na Mussa Omary Mkoyage.
Ruangwa waliojitokeza kuwania uenyekiti ni Ibrahim Ndoro, Beda Mbilla, Andrew Chikongwe, Litimbi Abdallah, Mussa Mtejela na Issa Libaba huku nafasi ya umakamu ikiwaniwa na Omary Songea, Mosses Mpwapwa na Fabian Nguli.
Lindi Vijijini waliojitokeza ni Makwinya Mathey Benino, Meinrad Mussa Ngombo, Rutamba na Mbonde Mussa Ahmaid Wilayani Kilwa waliojitokeza ni Ally Mohamed Mtopa anatetea kiti chake.

Moshi Mjini, Chadema kimewateua diwani wa Bomambuzi, Jaffary Michael, kuwania umeya wa Manispaa ya Moshi na diwani wa kata ya Kiborlon,Vicent Rimoi, kuwania unaibu meya.

Wednesday, November 24, 2010

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI WA JK HILI HAPA!

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI
1. Ofisi ya Rais (Utawala Bora) Mathias Chikawe

Ofisi ya Rais – Mahusiano na Uratibu: Stephen Wassira

2.Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma Hawa Ghasia

3. Ofisi ya Makamu wa Rais – ( Muungano) Samia Suluhu

2. Ofisi ya Makamu wa Rais – (Mazingira) Dr. Terezya Luoga Hovisa

4. Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge): William Lukuvi

2. Uwekezaji na Uwezeshaji Dr. Mary Nagu

5. Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Huruma Mkuchika

Naibu: Aggrey Mwanri

Naibu: Kassim Majaliwa

6. Wizara ya Fedha Mustapha Mkulo

Naibu: Gregory Teu

NAibu: Pereira Ame Silima

7. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Shamsi Vuai Nahodha

Naibu: Balozi Khamis Suedi Kagasheki

8. Wizara ya Katiba na Sheria Celina Kombani

9. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard K. Membe Naibu: Mahadhi Juma Mahadhi

10. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dr. Hussein Ali Hassan Mwinyi

11. Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dr. Mathayo David Mathayo

Naibu: Benedict Ole Nangoro

12. Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Naibu: Charles Kitwanga

13. Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka Naibu: Goodluck Ole Madeye

14. Wizara ya Maliasili na Utalii Ezekiel Maige

15. Wizara ya Nishati na Madini William Mganga Ngeleja 1. Adam Kigoma Malima

16. Wizara ya Ujenzi Dr. John Pombe Magufuli

Naibu: Dr. Harrison Mwakyembe

17. Wizara ya Uchukuzi Omari Nundu

Naibu: Athumani Mfutakamba

18. Wizara ya Viwanda na Biashara Dr. Cyril Chami

Naibu: Lazaro Nyalandu

19. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr. Shukuru Kawambwa

Naibu: Philipo Mulugo

20. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Haji Hussein Mpanda

Naibu: Dr. Lucy Nkya

21. Wizara ya Kazi na Ajira Gaudensia Kabaka Makongoro Mahanga

22. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Sophia Simba Umi Ali Mwalimu

23. Wizara ya Habari, Vijana na Michezo Emmanuel John Nchimbi

Naibu:Dr. Fenella Mukangara

24. Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samuel John Sitta

Naibu Dr. Abdallah Juma Abdallah

25. Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Prof. Jumanne Maghembe

Naibu: Christopher Chiza

26. Wizara ya Maji: Prof. Mark James Mwandosya

Naibu: Eng. Gerson Lwinge

Friday, November 19, 2010

Ya Peik, Mjengwa na Wanahabari kuhusu mafunzo ya ICT Arusha

Ya Peik, Mjengwa na Wanahabari kuhusu mafunzo ya ICT Arusha

NI takribani siku tano hivi, Vijana wa kazi ambao ni Waandishi wa habari wa Kanda ya Kaskazini (Nothern Zone) walikuwa katika darasa maalumu katika Jiji la Arusha wakijifunza ICT ili kwenda sambamba na wanataaluma wengine duniani.

Ilikuwa ni kuanzia Novemba 15 – 19 mwaka 2010,Majengo ya Summit Centre mjini Arusha ambapo kipo kituo cha Kompyuta ambalo ni tawi la Chuo kikuu cha Dar es Salaam (University of Dar es Salaam,Arusha Computer Centre) wanahabari walikuwa wakiumiza vichwa lakini wengine ilikuwa shida tupu!

Mada zilikuwa chini ya Mzungu Peik,raia wa Finland na Mwandishi wa Habari mkongwe wa kimataifa aliyebobea katika utangazaji upande wa Redio.

Ni hatua nzuri kwa wanahabari wetu lakini siamini na sitaki kuamini kama wote hizo Blogs zitakuwa active kwa muda wote.

Haya Misa Tanzania kazi kweni,Je! Mafunzo haya yataleta chachu?

Kiongozi Safari Hii ntakupelekesha ile mbaya au Huamini!

Thursday, November 18, 2010

Ghailani guilty over embassy bombing

 Ghailani guilty over embassy bombing

THE  first Guantanamo detainee tried in a US civilian court has been found guilty on just one out of 285 terror charges over the 1998 bombings of US embassies in Africa.

Tanzanian Ahmed Ghailani, 36, was found guilty of conspiracy to damage or destroy US property with explosives.

But he was cleared of many other counts including murder and murder conspiracy.

Ghailani faces a minimum of 20 years in prison. The verdict comes as the US weighs other civilian terror trials.
The source, says the verdict in the Ghailani case will be seen as a huge blow to the Obama administration.

It hopes to try other Guantanamo detainees in civilian courts - including alleged 9/11 mastermind Khalid Sheikh Mohammed.

Officials will now be considering how to proceed, but it could mean the controversial prison remains open for some time to come, our correspondent adds.
Witness barred
 
The attacks on US embassies in Tanzania and Kenya killed 224 people and were one of al-Qaeda's first international shows of strength.

Four accused co-conspirators were convicted over the bombings in 2001 and sentenced to life.

Analysis

The failure to convict Ahmed Ghailani on more of the charges will be viewed by some as proof that civilian courts are the wrong place to hold the Guantanamo trials.

Specifically there will be worries that the court threw out some evidence gained during enhanced interrogation at CIA "black sites".

Others will see that as a strength of the justice system.
The Obama administration is under pressure either way - either it reneges on its promise to close Guantanamo or risks the perception that suspected terrorists are being treated leniently.

Officials will now be considering how to proceed - but it could mean the controversial prison remains open for some time to come.
According to the indictment, Ghailani helped buy the Nissan lorry, oxygen and acetylene tanks used to destroy the US embassy in Dar es Salaam, Tanzania, and helped load boxes of explosives into the back of the lorry ahead of the bombing.

US investigators said Ghailani flew to Pakistan the night before the simultaneous bombings.

He was charged in the US in March 2001 but remained at large in Afghanistan and the Waziristan area of Pakistan, the US says. He was captured in July 2004 and transferred to Guantanamo Bay in 2006.

Last year, the US stayed proceedings in a military tribunal at Guantanamo Bay and transferred him to New York for the civilian trial.

Defence lawyers, meanwhile, argued Ghailani was only an errand boy who had been duped by al-Qaeda operatives, framed by contaminated evidence and knew nothing of the bomb plot.

After the verdict was announced on Wednesday night and the jury left the courtroom, the former Guantanamo Bay prisoner rubbed his face, smiled and hugged his lawyers. He will be sentenced on 25 January.

US Justice Department spokesman Matthew Miller said in a statement: "We respect the jury's verdict and are pleased that Ahmed Ghailani now faces a minimum of 20 years in prison and a potential life sentence for his role in the embassy bombings."
Ahmed Khalfan Ghailani
  • 1998: 224 die in US embassy bombings in Tanzania and Kenya
  • 2001: Ahmed Khalfan Ghailani included on FBI's new "Most Wanted Terrorists" list
  • 2004: Captured in Pakistan, and held at secret CIA facility
  • 2006: Moved to Guantanamo detention camp as "enemy combatant"
  • 2008: Charged before military commission over embassy bombings
  • 2009: Transferred to New York to face civilian charges
  • 2010: Acquitted of all but one (conspiracy) of 286 charges
During the trial, prosecutors suffered an early setback when federal Judge Lewis Kaplan in New York barred a key government witness from testifying, saying he had been named by Ghailani while the latter was "under duress".

Mr Ghailani was detained in Pakistan in 2004, taken to a secret CIA facility and then to Guantanamo Bay in 2006.

He was subject to what the government refers to as "enhanced interrogation" by the CIA. His lawyers say he was tortured.

Despite losing its key witness, the government was given broad latitude to refer to al-Qaeda and Osama bin Laden throughout the trial.

Defence lawyer Peter Quijano welcomed the acquittals. He said the one conviction would be appealed, adding: "We still truly believe he is innocent of all these charges."

Mtanzania Ahmed Khalfan Ghailani ana kesi ya kujibu

Ahmed Khalifan Ghailani ana kesi ya kujibu.

MSHITAKIWA wa kwanza kutoka gereza la Guantanamo Bay kutinga katika mahakama ya kiraia nchini Marekani, ana kesi ya kujibu baada ya upande wa mashitaka kumthibitisha kuhusika katika kula njama ya kushambulia kwa bomu mali ya taifa la Marekani.

Ghailani, raia wa Tanzania, alishtakiwa kwa kosa la kuhusika katika mashambulizi ya kundi la kigaidi la Al Qaeda, dhidi ya ubalozi wa Marekani nchini Kenya na Tanzania mwaka 1998.

Upande wa mashtaka katika kesi hiyo umesema kuwa Ahmed Ghailani, alichangia pakubwa katika maandalizi na mipango ya kundi la Al Qaeda ya kulipua balozi za marekani nchini Kenya na Tanzania.

Watu 224 waliuawa kufuatia mashambulio hayo mawili.

Mahakama hiyo ilifahamishwa kuwa Ghailani alinunua mitungi ya gesi zilizolipuka pamoja la lori iliyobeba vilipuzi hivyo.

Mtanzania huyo mwenye asili ya kisiwa cha Zanzibar, alikuwa anakabiliwa na mashataka 281 zikiwemo mauaji na jaribio la kuua.

Hatahivyo, Mahakama hiyo ilimpata bw Ghailani na hatia moja pekee ya kupanga kuharibu mali na majengo ya serikali.

Ushahidi uliokuwa umewasilishwa mbele ya mahakama hiyo ya Marekani dhidi ya mshukiwa huyo zimekataliwa na mahakama kwa sababu zilikusanywa na maafisa wa ujasusi wa Marekani CIA, katika magereza yasiyo rasmi nje ya Marekani kwa njia isiyofaa.

Maafisa hao wa ujasusi wanadaiwa kutumia mbinu kali kumhoji mshukiwa huyo,ikiwemo kumtesa ili akiri mashtaka dhidi yake na pia atoe habari zaidi.

Uamuzi huo wa mahakama unaonekana kuwa pigo kubwa kwa utawala wa Rais Barack Obama, wa Marekani na ahadi yake ya kuwafungulia mashtaka washukiwa wote wa ugaidi wanaozuiliwa katika jela la Guantanamo Bay, katika mahakama ya kiraia.

Maafisa wa serikali ya Marekani sasa wanachunguza upya jinsi ya kuendeleza kesi za washukiwa hao wa kigaidi, na hivyo kumaanisha jela hilo la Guantanamo Bay, iliyoko Cuba huenda isifungwe hivi karibuni.

WATU ZAIDI YA 90,000 IRINGA NI MBUMBUMBU WASIOJUA KUSOMA WALA KUANDIKA

WATU ZAIDI YA 90,000 IRINGA NI MBUMBUMBU WASIOJUA KUSOMA WALA KUANDIKA

Na Godfrey Mushi.

SERIKALI tayari imetangaza kwamba inakusudia kuifanya elimu ya kidato cha nne kuwa elimu ya lazima kwa kila mtanzania.

Ni mpango mzuri kwa ujenzi na ustawi wa taifa letu ambao kimsingi umelenga kumfanya kila mtanzania kupata elimu hiyo badala ya ile ya msingi ambayo huanzia darasa la kwanza hadi la saba.

Lakini ninachojiuliza kwa sasa ni kwamba, wakati tunapiga hatua hiyo, hivi ni wenzetu wangapi ambao hata hiyo elimu ya msingi hawakuipata na hawatarajii kuipata.

Nilimkariri Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Jumanne Maghembe hivi karibuni akiwa mkoani Kilimanjaro nyakati za kampeni akisema ya kuwa serikali imeamua kwamba kuanzia sasa elimu ya kidato cha nne itakuwa ya lazima.

Hakika nilistaajabu na kuhisi msisimko, ambao ulinifanya niperuzi baadhi ya kumbukumbu zangu katika mkoa mmoja tu wa Iringa kujua ni watu wangapi ambao bado ni mbumbumbu ambao hawajui kusoma,kuandika wala kuhesabu.

Niligundua serikali ilikuwa na wazo zuri kama ilivyoanzisha Shule za Sekondari za Kata ambazo kimsingi zimeonyesha mafanikio kwa kiasi fulani katika jamii yetu.

Katika mkoa wa Iringa kuna idadi ya zaidi ya watu 90,783 wasiojua kusoma,kuandika wala kuhesabu na hawatarajii kufikia kusudio la serikali ililotangaza hivi karibuni kwamba lazima elimu ya kidato cha nne iwe elimu ya lazima.

Ninafikiri serikali ingeweka pia mkazo katika kulinasua kundi hili katika umbumbumbu kwakuwa hawa nao ni wapiga kura na wamekuwa wakikosa haki zao mbalimbali au kushiriki mambo kadha wa kadha kutokana na kuona haya kwamba watashitukiwa wakienda huko maana hawajui kusoma wala kuandika.

Kwa mtazamo wangu ni lazima uwepo kwanza mkakati wa kupunguza idadi ya watu wasiojua kusoma, kuandika wala kuhesabu kwa kuanza kuwafundisha kilazima wananchi hawa kupitia mpango wa elimu ya watu wazima (MKEJA).

Ni lazima tuhakikishe kwamba watu hao wanaingia darasani kilazima kabla ya kutaka kila mtu awe na elimu ya kidato cha nne na zoezi hilo lihusishe wilaya zote ili kuwsaidia watu hao kuelimika kutokana na mabadiliko ya Sayansi na teknolojia.

Hakuna njia ya mkato ya kufuta ujinga zaidi ya kutumia njia aliyoianzisha hayati mwalimu, Julius Nyerere katika miaka ya 1970. Mwalimu Nyerere alihakikisha kila mwananchi asiyejua kusoma, kuandika wala kuhesabu aliingia darasani kufuta ujinga kupitia elimu ya watu wazima.

Bado kuna changamoto nyingi katika kufikia mafanikio ya mpango huo wa serikali kwakuwa mbali na mpango wa Mkeja, zaidi ya wanafunzi 1,298 wakiwemo wavulana 669 na wasichana 629 wamekosa elimu ya msingi katika umri unaostahili mkoani Iringa.

Ni vyema ukawepo mkakati wa kuhakikisha kwamba serikali inaongeza vituo kwa ajili ya wanafunzi wa MKEJA na MEMKWA ili waliokosa wapate elimu hiyo.

Utaratibu huo utakuwa ukiwasaidia wanafunzi hao kujiunga katika shule za kawaida za msingi na hivyo kuendelea na wasomo yao vizuri kama waliopo katika mpango maalumu wa shule za msingi.

BUNGE LA 10 LIWE CHACHU YA MABADILIKO YA KATIBA NA UUNDAJI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI.

BUNGE LA 10 LIWE CHACHU YA MABADILIKO YA KATIBA NA UUNDAJI WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI.

Na Godfrey Mushi
IDADI ndogo ya wananchi waliojitokeza kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu pamoja na dosari nyingine zilizojitokeza wakati wa zoezi hilo, hakika zimedhihirisha kwamba Tanzania tunahitaji chombo huru cha kusimamia chaguzi zetu ili kuzifanya ziwe huru na za haki.

Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) ya sasa iliyopo chini ya Jaji Lewis Makame, si huru na inaundwa na kada zinazohusisha hata watumishi wa umma ambao wanaitii serikali ya Chama cha Mapinduzi.

Wapo watakaochelewa kuamini haya yanayopiganiwa na wanaharakati kuhusu kuundwa kwa Tume huru ya Taifa ya uchaguzi baada ya uchaguzi mkuu wa sasa kumalizika.

Hakuna asiyetambua kwamba Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya,Miji,Manispaa na Majiji walikuwa maajenti wa NEC kama wasimamizi wa uchaguzi mkuu.

Ukiwaacha hao wamo pia Watendaji wa Kata ambao ni Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi lakini wengi wao ni makada na wakereketwa wakutupwa wa CCM, sasa tutawaaminije kwamba wanaweza kutenda haki pale chama tawala kinaongoza serikali kinaposhindwa.

Wote hawa ni watendaji wa Serikali na wanafanya kazi kwa kufuata maelekezo ya mwajiri yaani serikali iliyo chini ya chama tawala (CCM),hakika hawawezi kumwangusha aliyewaweka hapo labda NEC ivunjwe na kuundwa mpya ambayo haitahusisha watendaji wa umma.

Swali la kujiuliza ni kwamba, nani kati ya hawa wenzetu atakubali kuadhibiwa na aliyemwajiri kwa sababu maelekezo aliyopewa hakutekeleza (kuisaidia CCM ishinde)...hakika hakuna atakayebukali hilo akikumbuka kilichomnyoa kanga manyoya shingoni.

Ni wazi kwamba tunahitaji tume huru ambayo viongozi na watendaji wake, watafanya kazi zao bila ya kuhofu kupoteza kazi zao kama hawatakisaidia chama tawala kwa namna moja au nyingine.

Ipo haja ya kuundwa kwa tume hiyo ambayo watendaji wake, hawatafungwa na kitanzi cha uaminifu na uadilifu ama uwezo wao kutiliwa shaka na umma wa watanzania.

Tumeshuhudia udhaifu pale Tume ilipotangaza matokeo ya kura za Rais katika jimbo la Geita ambapo ilitangaza aliyekuwa akiwania kiti hicho kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk.Wilbrod Slaa kwamba amepata kura 3,750 badala ya kura 25,000 na ushehe hivi.

Tafsiri hii ya makosa yakutiliwa shaka inawakatisha tamaa wapiga kura na ni mojawapo ya vitu vinavyowafanya baadhi ya watu waamini kwamba NEC inatumika kuisadia CCM.

Tanzania inakadiriwa kuwa na watu zaidi ya milioni 44 kwa sasa lakini kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC),waliojiandikisha kupiga kura na kushiriki uchaguzi mkuu uliopita walikuwa watu milioni 20.1 sawa na asilimia 42.

Wachache walio katika madaraka na pengine ndani ya Chama cha Mapinduzi, wanaweza wasione umuhimu wa kufanyika kwa mabadiliko haya kwakuwa wengi wao hawaguswi na hisia za umma kuhusu hoja ya kuundwa kwa tume huru.

Yupo mwanadiplomasia mmoja aliwahi kusema ‘namnukuu’ “watu wengi wanadhani kwamba kero zao zinaweza kuondoka kwa kufanya kero…lakini kero huondoka kwa kuzielewa,kuzijadili na kuzitafutia ufumbuzi tena kwa juhudi na maarifa”.

Jirani zetu Kenya, wamefanikiwa kuwa na Tume huru ya uchaguzi baada ya ile iliyokuwa ikiongozwa Samweli Kivuitu kuvunjwa baada ya kusababisha machafuko na mauaji ya raia baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.

Tume hiyo ilikuwa ikituhumiwa kuhusika katika uchakachuaji wa matokeo ya nafasi ya rais wa nchi hiyo kwa kumrejesha madarakani Rais wa sasa, Mwai kibaki aliyekuwa amekataliwa na Wakenya.

Si dhani kama ni busara kwa watawala wetu kusubiri yatokee kama yaliyotokea nchini Kenya ndo waone umuhimu wa kuunda tume huru ya uchaguzi.

Ni vizuri tukajipanga sasa na kuanza mchakato wa kuhakikisha kwamba Serikali ya Rais Jakaya Kikwete inachukua jukumu la kuunda tume mpya ya uchaguzi ambayo itakuwa huru.

Mathalani,vyama vya upinzani vimekuwa vikilalamikia mara kadhaa Katiba ya nchi iliyopo pamoja na uteuzi wa maofisa wa tume ya taifa ya uchaguzi.

Ni jambo la busara na hekima kuona mambo haya mawili hayabinafsishwi na watawala kwa maana kwamba, tunataka yapewe uwanja mpana wa kujadiliwa na kufikiwa mwafaka na jamii yote.

Wabunge wetu tuliowachagua ni vyema wakafunga kibwebwe katika kulipigania hili la kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi pamoja na mabadiliko ya katiba, kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu mwingine ifikapo mwaka 2015.

Wachunguzi wa masuala ya kisiasa hapa nchini,wasema kuwa sababu kubwa ya wananchi kutojitokeza kupiga kura katika uchaguzi mkuu uliopita wa Oktoba 31 mwaka huu ulisababishwa na wapiga kura kufohia utendaji wa tume ya taifa ya uchaguzi ndio maana hawakujitokeza kwa wingi kama ilivyotarajiwa.

Kwa mtazamo wangu kutokana na hoja zinazotolewa na wanaharakati wakiwemo wapinzani wa Chama cha Mapinduzi ni vyema mabadiliko ya katiba yakafanyika na kuruhusu uundwaji wa tume huru ambayo haitakuwa ikilalamikiwa na kuona kama inakilinda chama tawala.

Katika hili ni busara tukaweka maslahi ya Taifa mbele kwa sababu inawezekana ikawa ni sababu mojawapo iliyowafanya wananchi wasijitokeze kupiga kura katika uchaguzi mkuu uliopita.

Mmoja wa wanasiasa wa siku nyingi na kada wa CCM mkoani Iringa,David Butinini aliwahi kuniambia siku moja kwamba, ili ipatikane tume huru ya uchaguzi hapa nchini,

itatulazimu kuweka mazingira ambayo yatafanya kila mtu aone kwamba ni mazingira mazuri yasiyo na shaka na kwa namna moja au nyingine, wananchi walishirikishwa kuyaandaa kwa maana ya namna ya kupata katiba mpya na jinsi ya kuchagua tume ya uchaguzi.

“Inawezekana tume ikawa ni ya watu waadilifu lakini kama taratibu za uteuzi wake zinatoa mwanya wa kutokuwa na imani nayo,basi hiyo kasoro inaweza ikafanya watu waone ni kubwa…Hivyo,kwa namna moja au nyingine inaweza ikapunguza ushiriki katika zoezi la upigaji kura za kuwachagua viongozi wetu kama tulivyoona katika uchaguzi mkuu uliopita”,anasema Butinini.

Novemba 12 mwaka huu, umma wa Watanzania ulishuhudia wabunge wateule 327 wakila kiapo katika ukumbi wa bunge mjini Dodoma baada ya wabunge kupiga kura ya kumchagua Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anna Semamba Makinda (Mbunge wa Njombe Kusini).

Makinda alishinda baada ya kuchaguliwa kwa kura 265 katika ya kura 327 zilizopigwa na kumwangusha mpinzani wake Mwanasheria mashuhuri Maberere Marando aliyepata kura 53.

Kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa Spika, Makinda alisema kuwa anataka bunge la 10 liwe ni bunge moja litalalofanya kazi kwa karibu na wabunge wote kwa maslahi ya watanzania na si ya watu binafsi.

Kwa mantiki hiyo,tunategemea bunge hilo litamaliza kiu ya watanzania ya kutaka kuwepo kwa mabadiliko ya katiba ambayo itapelekea kufumiliwa kwa NEC na kuundwa kwa tume mpya ambayo itakuwa tume huru na ya haki kwa vyama vyote.

Vivyo hivyo,tunawategemea wabunge wanaounda kambi ya upinzani bungeni wakati ukifika wapenyeze hoja ya kuifumua katiba ya nchini pamoja na tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) ili iundwe mpya itakayokuwa haiteuliwi na Rais kama hii iliyopo hivi sasa.

Safari hii kambi ya upinzani bungeni inaongozwa na chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutokana na kuwa na wingi wa wabunge.ina wabunge 45 ikifuatiwa na chama cha wananchi CUF chenye wabunge 34 huku TLP na UDP vikiwa na mbunge mmoja mmoja.

Safu hiyo inaongozwa na mbunge wa Jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro Freeman Mbowe na Naibu wake Zitto Kabwe,mbunge wa Kigoma Kaskazini na Mnadhimu mkuu wa kambi hiyo Mwanasheria, Tundu Lissu ambaye ni mbunge wa Singida Mashariki.

Hawa ni miongoni mwa askari wanaotegemewa katika mapambano dhidi ya serikali katika kuhimiza yafanyike haraka mabadiliko ya katiba yatakayotoa fursa ya kuundwa kwa tume mpya ya uchaguzi itakayo kuwa huru nay a haki ambayo haitaingiliwa utendaji wake kwa namna moja au nyingine.

Godfrey Mushi ni mwandishi wa Gazeti la Nipashe mkoani Iringa,anapatikana kwa simu namba 0715 545490 ama barua pepe, ghandsome79@hotmail.com

Anguko la mawaziri, wakuu wa mikoa funzo kwa wabunge

Anguko la mawaziri, wakuu wa mikoa funzo kwa wabunge

Na Godfrey Mushi
Kuna mwana diplomasia mmoja hapa nchini, aliwahi kusema, namnukuu; “kama wewe hauhitaji mabadiliko, basi ujue wewe ni mwathirika wa mabadiliko.”

Dhana ya mwanadiplomasia huyo inaweza kufanana na fikra nyingine kwamba, viongozi wa umma ni mfano wa marubani…hawaruhusiwi kubeba abiria bila kufuzu.

Rubani anapofikia hatua ya kurusha ndege angani, hawezi kusahau kwamba upo wakati atalazimika kutua ardhini, iwe ni kutokana na kuishiwa mafuta, hitilafu au kutua kwa usalama.

Ndivyo ninavyoweza kuzungumzia anguko la baadhi ya `vigogo’ wa siasa waliokuwa katika nyadhifa za uwaziri na ukuu wa mikoa, lakini wakashindwa kutetea ubunge wao.

Lakini wapo `vigogo’ wengine waliokuwa maarufu sana katika siasa za nchi hii. Hawakuwa mawaziri ama wakuu wa mikoa. Lakini wameshindwa vibaya. Wameanguka katika kuwania ubunge.

Zipo sababu nyingi zinazotajwa kuwa chanzo cha anguko la `vigogo’ hao, lakini kwa ujumla wake, hatua hiyo inaonekana dhahiri kuwa ni viashiria vinavyothibitisha kujisahau kwao, kusahau wajibu wao hasa kwa wapiga kura katika kipindi walipokuwa wabunge.

Waliposhika nyadhifa za juu ama kupata umaarufu wa kisiasa, wakasahahu kwamba asili yake ni wananchi walio katika mahitaji ya kuvushwa salama kutoka katika umasikini unaowakabili na kwenda katika ustawi bora wa maisha.

Walishindwa (tena inawezekana ni kutokana na uzembe ama dharau), kurejea kwa wananchi, kukaa na wapiga kura wao, kuzungumza nao, kupanga na kushirikishana namna bora ya kujiletea maendeleo.

Hawakurudi kwa wananchi ili kueleza mambo mema waliyoyafanya na changamoto zilizowakabili. Wakajiona na kuamini kwamba `wao ndio wao’.

Kana kwamba haitoshi, inawezekana waliendelea kuota njozi, kuwa watadumu katika uongozi wa umma mpaka watakapoitwa na Mwenyenzi Mungu.

Umma umewashuhudia `vigogo’ wakishindwa kunadi sera za chama tawala-Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichowateua kwa kuwaamini, kwamba wangekipatia ushindi katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

Zipo taarifa na vielelezo vinavyothibitisha jinsi miongoni mwa `vigogo’ hao waliposhindwa kuzinadi sera na ilani ya CCM, badala yake wakaendeleza mashambulizi binafsi na kashfa dhidi ya wagombea wengine.


Hakika, anguko la `vigogo’ wa CCM na kufufuka kwa upinzani nchini, kumetokana na wananchi kuchoshwa na ubabaishaji wa baadhi ya viongozi ndani ya CCM na serikali yake, kutofikiwa kwa matarajio ya umma, kushamiri kwa ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.
Hadi sasa wapinzani wameweza kusonga mbele na kunyakua majimbo mengi zaidi kuliko ilivyokuwa tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi, 1992.

Inashangaza kuona wapo baadhi ya watu wasiokubali kuwepo kwa mabadiliko hayo. Watu wa aina hiyo wanaamini kwamba ikiwa upinzani utashinda na kutwaa madaraka, kuna uwezekano wa kutokea machafuko.

Na wapo wengine wanaoamini kwamba asipochaguliwa mgombea ubunge kupitia CCM, eneo la jimbo husika litatengwa na serikali na kukosa miradi ya maendeleo na ustawi wa jamii.

Ilitarajiwa kwamba wagombea wakiwemo `vigogo’ walioangushwa, wangejikita zaidi katika kuelezea sera, ilani za vyama vyao na kutoa taarifa sahihi ya utekelezaji wa ahadi za kipindi kilichopita.

Lakini walizigeuza kampeni kuwa sehemu ya kufanya siasa za kuzungumzia maslahi binafsi na kuchukua muda mwingi kuwatuhumu waliojitokeza kidemokrasia kupambana nao.

Hata hivyo, baada ya kushindwa katika Uchaguzi Mkuu katika nafasi mbalimbali za uongozi wa kuchaguliwa, iwe urais, ubunge, udiwani ama ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, ni wakati wa kukaa na kutafakari changamoto zilizojitokeza na kuchangia kushindwa kwao, ikiwezekana kujipanga upya.


Mkoani Iringa

Lakini katika mkoa wa Iringa, tulishuhudia majimbo matatu kati ya 11 `yakiwaka moto’ kutokana na kiwango kikubwa cha ushindani wa kisiasa wakati wa kampeni.

Hali ilisababisha kuibuka kwa utabiri usiokuwa rasmi, kwamba kutakuwa na anguko kubwa la `vigogo’ waliokuwa wakitetea nafasi zao za ubunge.

Majimbo hayo ni Njombe Magharibi lililokuwa na mgombea wa CCM, Gerson Lwenge (kwa sasa mbunge mteule) aliyeshinda kwa kura 29,743 dhidi ya Thomas Nyimbo wa Chadema aliyeshika nafasi ya pili kwa kupata kura 13,483.

Majimbo mengine ni Njombe Kaskazini ambalo lilikuwa na mgombea wa Chadema, Alatanga Nyagawa na Deo Sanga ambaye kwa sasa ni mbunge mteule na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa.

Licha ya CCM kupata ushindi katika majimbo hayo, lakini upepo wa mabadiliko ulishamirisha ushindani hadi katika majimbo ambayo `vigogo’ wa chama tawala walianguka.

Hali hiyo ilionekana katika majimbo kama la Iringa Mjini ambalo lilikuwa na wagombea wa vyama vitatu vya siasa, akiwemo Mbega wa ambaye pamoja na Mariam Mwakingwe wa NCCR-Mageuzi,walishindwa na Mchungaji Peter Msigwa wa Chadema.

Zipo sababu nyingi zilizotolewa kuhusu kutokukubalika kwa Mbega, mojawapo ikiwemo ni kutoonekana jimboni kwa muda mrefu.

Hata hivyo, Mbega alijitetea mara kadhaa kwamba kasoro hiyo na nyingine zilizoelekezwa kwake, zilitokana na kuangushwa na wasaidizi wake, aliowaacha jimboni humo, lakini wakashindwa kutekeleza wajibu wao.

Monica, aliangushwa baada ya Mchungaji Msigwa kupata kura 17,742 kati ya kura 35,910 zilizopigwa, huku Mbega akiambulia kura 16,916 na Mwakingwe akipata kura 950.

Iringa Mjini ni sehemu moja ya majimbo yaliyoshuhudia `vigogo’ wakiangushwa katika nafasi za ubunge.

Imedhirika kwamba hivi sasa kuna wapiga kura wasiokubali kuyumbishwa katika kufikia uamuzi unaokidhi maslahi ya umma.

Mathalani Wahehe wana desturi ya kutumia msemo unaosema, ‘nene swela’, yaani ‘mimi basi’, wakiwa na maana kwamba hawakubaliani na mtu fulani, lakini hapo unaweza kuwa nao na wasikuonyeshe kama wanafikiria kutumia neno hilo mbele yako.

Majimbo mengi likiwemo la Iringa Mjini yana wapiga kura wenye tabia ya kubadili viongozi wa kuchaguliwa bila kujali vyama wanavyotoka, ili mradi wanabaini kwamba kiongozi aliyepo hakidhi matarajio yao.

Mathalani, mwaka 1995 Iringa Mjini lilichukuliwa na wapinzani kama ilivyo sasa, likiwa chini ya Faramagoha Kibasa aliyekuwa NCCR-Mageuzi.

Ushindi huo ulipatikana dhidi ya Hans Kitine, bosi wa zamani wa usalama wa taifa, aliyekuwa mgombea ubunge kupitia CCM.

Vivyo hivyo safari hii imekuwa ni zamu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuliwakilisha jimbo hilo, baada ya kuwashinda wapinzani wake akiwemo Mbega wa CCM.
Changamoto kwa washindi

Wanasiasa waliowaangusha `vigogo’ katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, wanapaswa kubaini kwamba mahitaji na matarajio ya umma kwa wabunge wao bado yapo.

Kwa kadri walivyokuwa wanahitaji kutoka kwa `vigogo’ hao, ndivyo watakavyohitaji kutoka kwao na kwamba wasipotimiza matakwa hayo, wasitegemee kuikwepa adhabu iliyowapata `vigogo’ husika.

Mfano halisi umeonekana katika jimbo la Iringa Mjini katika kipindi cha kuanzia Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa vyama vingi uliofanyika mwaka 1995.

Katika kipindi hicho, wapiga kura wameshawachagua wabunge kutoka vyama vya NCCR-Mageuzi, CCM na sasa Chadema.

Wanapaswa kuyatambua makundi mbalimbali ya kijamii hasa wanawake na vijana walioshiriki kikamilifu kuwapigia na kulinda kura kiasi cha kufanikisha ushindi walioupata.

Zipo ahadi kadhaa zilizotolewa na washindi, miongoni mwa hizo zikiwa ndani ya ilani za vyama vyao na nyingine zikitokana na mahitaji ya papo kwa hapo.

Zote hizo zinastahili kuwekwa katika kumbukumbu na kutekelezwa, kama ilivyokuwa kwa Mchungaji Msiwa alipoahidi, kwamba baada ya kuapishwa na kuanza kazi ya uwakilishi bungeni, ataweka Mwanasheria katika ofisi yake, ili ashughulikie matatizo mbalimbali ya wananchi.

Ahadi nyingine ilikuwa ni kushirikiana na uongozi wa halmashauri ya manispaa ya Iringa, kutatua matatizo ya ardhi, upimaji wa viwanja, kuongeza na kupanua huduma za ughani kwa jamii ya wafugaji, wakulima na kufufua sekta ya utalii.

Prof. Wangari Maathai

Its wonder full to see woman get a higher education in East Afrika like Wangari Muta Maathai who was born in Nyeri, Kenya (Africa) in 1940. The first woman in East and Central Africa to earn a doctorate degree, Professor Maathai obtained a degree in Biological Sciences from Mount St. Scholastica College in Atchison, Kansas (1964). She subsequently earned a Master of Science degree from the University of Pittsburgh (1966). Professor Maathai pursued doctoral studies in Germany and the University of Nairobi, obtaining a Ph.D. (1971) from the University of Nairobi where she also taught veterinary anatomy. She became chair of the Department of Veterinary Anatomy and an associate professor in 1976 and 1977 respectively. In both cases, she was the first woman to attain those positions in the region.

Monday, November 15, 2010

HEY, JAMBO TANZANIA !

HEY, JAMBO TANZANIA !

My name is Godfrey Mushi. Am working with Nipashe and the Guardian Newspapers in Tanga Region. Am 30 years of age and i have family stil in Tanga. I hope this training of Internet for Journalist can make the Journalist to understand many things concerning their work.For example today we are lerning how to buy a ticket through intenert,maps and banks. The workshop continued in University of Dar es Salaam,Computing Centre in Arusha Region.